Wednesday, July 13, 2011

MAREKANI YAONYA RAIA WAKE KWENDA SUDAN KUSINI

Marekani inawaonya raia wake
hatari ya kusafiri kuelekea Sudan
Kusini licha ya maadhimisho ya
uhuru katika nchi hiyo mpya.
Ubalozi wa Marekani nchini
Sudan kusini uliwasihi
wamarekani Jumanne kutosafiri
kuelekea mikoa ya mpakani kati
ya Sudan na Sudan kusini
ikielezea mapigano ya karibuni
kati ya majeshi yanayotii wakuu
wa nchi hizo mbili pamoja na
kuongezeka kwa majeshi pande
zote za mpaka.
Ubalozi unasema ukiongezea
mapigano hayo ya ardhini, jeshi
la anga la Sudan limepiga
maeneo ya mpaka katika
majimbo ya Unity na Kordofan
kusini. Ubalozi pia umeonya
hatari ya ghasia katika maeneo
yote ya Sudan kusini ikisema
kuna majeshi tofauti ya waasi
yasiyopungua saba ambayo mara
kwa mara yanapambana na
majeshi ya Sudan kusini.
Ubalozi unasema serikali ya
Sudan kusini ina uwezo kiasi wa
kupambama na uhalifu nje ya mji
mkuu wa Juba na kwamba hata
hapo walipo hatari ya ghasia za
uhalifu zipo juu.
Sudan kusini imekuwa taifa jipya
siku ya Jumamosi baada ya
wakazi wake walipopiga kura
kwa wingi kujitenga kutoka
kaskazini katika kura ya maoni ya
mwezi Januari.
Sudan ilipigana vita vya wenyewe
kwa wenyewe kwa miaka 21
ambavyo vilimalizika mwaka
2005. Sudan na Sudan kusini
bado wana mizozo kadhaa
ambayo haijatatuliwa ikiwemo
nani atadhibiti mkoa wa Abyei
wenye utajiri wa mafuta na
namna ya kushirikiana katika
mapato ya mafuta.

No comments:

Post a Comment