Wednesday, July 27, 2011

SERIKALI IMEONGEZA TSH.2100 KATIKA MSHAHARA

SERIKALI imeongeza mshahara
wa sh 2,100 kwa watumishi
wake wa kima cha chini na sh
86,000 kwa wafanyakazi wa
ngazi ya juu.
Kwa mujibu wa taarifa
iliyotolewa kwa vyombo vya
habari jijini Dar es Salaam jana,
kima cha chini kimekuwa sh
150,000 badala ya sh 135,500
huku kima cha juu kikiwa sh
2,158,000 badala ya 1,895,740
kwa mwezi.
Kupitia taarifa hiyo Katibu Mkuu
wa Ofisi ya Rais Menejimeti ya
Utumishi wa Umma, George
Yambesi, alisema mbali na
ongezeko la asilimia 11, kuna
watumishi wengine
wameongezwa kwa wastani wa
asilimia 8.6.
Alisema mbali na kima cha chini
kuongezwa kwa sh 2100 ambao
ni ngazi ya TGTS A.1 hadi TGTS
A.8, wapo watumishi wengine
waliopata nyongeza ya sh 5,200
kutoka ngazi ya TGTS B .1 hadi
TGTS B.8.
Akitaja ngazi zingine za
mishahara kuwa ni pamoja na
ngazi ya TGTS C.1 hadi TGTS C.12
waliongezewa sh 7,000.
Aidha alisema ngazi ya TGTS D.1
hadi TGTS D.10 wameongezewa
sh 9,100, ngazi ya TGTS E.1 hadi
TGTS E .10, sh 12,000; ngazi ya
TGTS F.1 hadi TGTS F. 10 sh
20,600; ngazi ya TGTS G.1 hadi
TGTS G.12, sh 23,200; na ngazi ya
TGTS H.1 hadi TGTS H. 12, sh
42,000.
“Marekebisho haya yanawahusu
watumishi wa serikali kuu,
watumishi wa serikali za mitaa,
watumishi walioshikizwa
kwenye taasisi za umma pamoja
na watumishi ambao watakuwa
kwenye likizo inayoambatana na
kuacha kazi au kumaliza
mikataba baada ya Julai mwaka
huu,” alisema Yambesi kutipia
taarifa hiyo.
Aidha alisema watumishi
wanaopata mishahara binafsi
ambayo ni mikubwa kuliko ile ya
vyeo vyao halisi watahusika na
marekebisho haya iwapo vyeo na
mishahara yao itaangukia katika
vyeo na ngazi mpya za
mishahara.

No comments:

Post a Comment