Thursday, June 30, 2011

MADIWANI JINO KWA JINO NA DK SLAA

MADIWANI wa Chadema katika
Manispaa ya Arusha, wamesema
chama hicho ‘hakina ubavu’ wa
kuwafukuza kwa kuwa kufanya
hivyo, kitakuwa kinacheza
mchezo wa pata potea.
Wakizungumza na Gazeti la Habari leo la nchini Tanzania kwa
masharti ya kutotajwa majina
gazetini baada ya kuonywa
kutozungumzia mgogoro wao
na uongozi wa chama hicho
Taifa, madiwani hao walisema
wanaamini Kamati Kuu ya chama
hicho haiwezi kufanya kosa hilo.
‘’Hili suala linapaswa kuamuliwa
kwa hekima na busara,
kunifukuza mimi ama madiwani
wote hapa kuna mambo mawili;
moja Chadema kupoteza viti
vyote ama kupata na hiyo ni
bahati nasibu na sidhani kama
Kamati Kuu italikubali hilo,’’
alisema mmoja wa madiwani
hao.
Juni 29 Katibu Mkuu wa
Chadema, Dk. Willibrod Slaa,
alikaririwa akisema chama hicho
kiko tayari kuwatimua madiwani
wake wote wa Arusha kwa
madai kuwa wamekisaliti chama
baada ya kufikia muafaka wa
Arusha kwa maslahi ya mkoa
huo.
Dk. Slaa alikaririwa, akisema
uamuzi wa madiwani huo,
kumpata meya na naibu wake
Arusha ambao ulipongezwa na
Baraza la Vijana la Chadema
(Bavicha), hawautambui kwa
madai una upungufu ukiwamo
wa kukosa barua ya Chadema ya
kukubali maridhiano.
Baada ya kauli hiyo ya Dk. Slaa,
iliyotolewa baada ya kauli
nyingine ya Mbunge wa Arusha,
Godbless Lema, kwamba
hatambui maridhiano hayo ya
amani na yenye lengo la
kuharakisha maendeleo ya
Arusha, madiwani hao Juni 30
waliweka kikao katika hoteli
moja
kubwa mjini hapa kujadili kauli
hizo.
Baada ya kikao hicho, diwani
mwingine alisema Dk. Slaa
amewatumia ujumbe kwa njia ya
mtandao wa intaneti na
kuwaamuru waache
kuzungumzia suala hilo katika
vyombo vya habari.
Alisema hata hivyo, kikao chao
kimesisitiza kuwa muafaka
waliofikia na madiwani wenzao
wa CCM, ni sahihi uliofuata
taratibu zote kwa maslahi ya
chama na si uamuzi wa mtu
binafsi wenye uroho wa
madaraka na kamwe
hawakukurupuka.
‘’Tumefikia muafaka kwa maslahi
ya Chadema pia, hatukufanya
hivyo kwa uroho wa kutaka vyeo
katika kamati ndani ya
Halmashauri.
Kauli kwamba tuliamua kwa
uroho wa madaraka ni kutaka
kuupotosha umma na kauli hizo
hazifai kutamkwa na kiongozi
kama Lema,’’ alisema diwani
huyo.
Alisema wanawaheshimu sana
viongozi wao wa juu, lakini na
wao ni viongozi waliochaguliwa
na wananchi kama Lema na
uamuzi waliochukua Lema
anaujua, lakini inasikitisha kuona
madiwani wakiamua ni kosa,
wakati ni kwa maslahi ya wakazi
wa Arusha.
Diwani huyo alidai Lema anajua
kila kitu, kwa kuwa katika
mchakato wa awali,
alishirikishwa na kuambiwa kila
kitu kinachoendelea, lakini
hakutoa uamuzi ila
kinachoonekana ni ubinafsi
wake na huo ndio unaosumbua
ndani ya Chadema.
‘’Hapa suala ni kutoa uamuzi kwa
maslahi ya chama na si mtu
binafsi; hilo halitawezekana,
kwani kila mmoja anapaswa
kuheshimiwa na kusikilizwa
katika kutoa uamuzi na
wasitokee baadhi ya watu ndani
ya chama kuonekana miungu
watu,’’ alisema.
Mbali na Dk. Slaa na Lema, pia
Mwenyekiti wa Chadema,
Freeman Mbowe, alinukuliwa
kwa nyakati tofauti akipinga
muafaka huo.
KWA HABARI ZA UHAKIKA ZAIDI SOMA GAZETI LA HABARI LEO!

Sunday, June 26, 2011

AZALILISHWA KWA KUDUNGWA SINDANO SEHEMU YA HAJA KUBWA

JESHI la Polisi mkoani Rukwa
linamtafuta mwanamke mmoja
mkazi wa mtaa wa Lwiche
Kitongoji cha Mazwi katika
Manispaa ya Sumbawanga kwa
tuhuma ya kumchoma sindano
iliyowekwa maji ya moto mtoto
mwenye umri wa miaka sita
kwenye sehemu yake ya haja
kubwa kwa madai kuwa ni
kikojozi.
Mwanamke huyo aitwaye Severia
Mpepo anatuhumiwa kumfanyia
unyama huo mtoto huyo na
kumsababishia maumivu makali
juzi majira ya saa moja asubuhi.
Kitendo hicho kisicho kawaida
kilisababisha mtoto huyo ambaye
ni wa kiume kupiga kelele za
kuomba msaada kutoka kwa
majirani kabla ya kuzimia na
kukimbizwa na wasamaria katika
Hospitali ya Mkoa wa Rukwa kwa
ajili ya matibabu.
Kwa mujibu wa majirani wa
mtoto huyo ambao hawakutaka
kutajwa majina yao walisema
kuwa tukio la kuunguzwa
linafuatia mateso mfululizo
aliyokuwa akiyapata kutoka kwa
mama mlezi wake, Severia
ambaye amekuwa akimlea kwa
kipindi cha miezi sita tangu
kufariki kwa mama mzazi wa
mtoto huyo.
Majirani hao walisema mtoto
huyo aliletwa kwa mlezi huyo na
babake mzazi anayefahamika
kwa jina la Peter Matalanganya
kufuatia ushauri wa rafiki yake
ambaye ndiye mume wa Severia
aliyemshauri kuwa ampeleke
kwake ili apate kumlea baada ya
mkewe kufariki dunia.
“Tunasikia kuwa huyu mtoto
aliletwa hapa na babake miezi
sita iliyopita baada ya mamake
kufariki, lakini kuanzia alipofika
huyu mwanamke amekuwa
akimtesa sana mara amnyime
chakula, mara amchape na juzi
ndio kahitimisha kwa kumfanyia
huu unyama wa kumwunguza
katika sehemu yake ya haja
kubwa, kwa kweli huyu mama
hafai na ni muuaji mkubwa,“
walisema majirani hao.
Kwa upande wake Mganga Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa, Dk. Saduni
Kabuma alikiri kumpokea mtoto
huyo hospitalini hapo na
kupatiwa tiba ambapo katika
uchunguzi alionekana kuwa
ameunguzwa katika sehemu za
haja kubwa na maji hayo kiasi
cha kumsababishia
malengelenge.
Dk. Kabuma alisema kuwa taarifa
alizopata kutoka kwa ndugu wa
karibu waliomfikisha hospitalini
hapo zimedai mama mlezi wa
mtoto huyo alichukua uamuzi
huo wa kinyama kwa kuwa
kijana ni kikojozi wa kupindukia.
Naye Daktari aliyempokea mtoto
na kumpatia huduma ya
matibabu katika kitengo
wagonjwa wa nje, Dk. Revocatus
Kasoni alisema kuwa hali ya
mtoto huyo inaendelea vizuri na
kuongeza kuwa bado yupo
katika uchunguzi wa kitabibu
zaidi.
Alipoulizwa na waandishi wa
habari waliofika nyumbani
kwake kutaka kufahamu undani
wa tukio hilo alikiri kutenda
unyama huo, lakini alisema
hakutenda kwa makusudi bali
alikuwa anampatia mtoto huyo
tiba ya ugonjwa wa tumbo kwa
kumpiga bomba.
Kamanda wa Polisi mkoani
Rukwa Isuto Mantage
alipoulizwa kuhusu tukio hilo
alisema kuwa mama huyo bado
hajakamatwa na Jeshi hilo
linaendelea kumsaka mama huyo
ili sheria ichukue mkono wake
iwapo ikibainika kuwa alitenda
uovu huo.
....

Thursday, June 23, 2011

TATIZO LA MISHAHARA KWA WALIMU KUISHA MWAKANI

KUANZIA mwaka ujao wa fedha,
walimu wa shule za msingi na
sekondari hawatapata tena
matatizo ya kupata mishahara
mara wanaporipoti kazini.
Katibu Mkuu wa Tamisemi,
Hussein Kattanga amesema,
mwaka huu yametokea matatizo
ambayo yalisababisha baadhi ya
walimu kushindwa kulipwa
mapema mishahara yao ndio
maana yakatokea matatizo hayo.
“Tumejipanga kuhakikisha kuwa
mwalimu anaporipoti katika
kituo chake cha kazi analipwa
stahili zake zote,” amesema
Kattanga.
Amesema, wakurugenzi
watendaji watapelekewa fedha
hizo haraka na kwenye mfumo
wao wa malipo utakuwa
umeunganishwa moja kwa moja
Wizara ya Utumishi pamoja na
Fedha.
Alikuwa akizungumza kuhusu
maadhimisho ya Siku ya Serikali
za Mitaa mwaka 2011 ambayo
kitaifa yatafanyika mkoani
Rukwa Julai mosi mwaka huu na
mgeni rasmi atakuwa Waziri
Mkuu Mizengo Pinda.
Alisema, maadhimisho hayo
yatazinduliwa leo na Mkuu wa
Mkoa wa Rukwa, Daniel ole
Njoolay mjini Sumbawanga.
Alifafanua kuwa lengo la Serikali
kugatua madaraka na kuziweka
shule hizo kwenye ngazi ya
halmashauri ni kutaka kutatua
matatizo kama hayo ya walimu
kwa haraka.
Alisema, licha ya sherehe ya
kitaifa kufanyika Sumbawanga,
lakini kila halmashauri itafanya
sherehe hizo katika eneo lao ili
kutoa fursa ya wananchi wa
maeneo husika kwenda kutoa
kero zao.
Alitoa mwito kwa wananchi
kujitokeza kwa wingi katika
maeneo ambako sherehe hizo
zitafanyika ili waelimishwe haki
zao na majukumu ya Serikali za
Mitaa.
Kaulimbiu ya maadhimisho ya
mwaka huu ni mafanikio ya
Serikali za Mitaa katika miaka 50
ya Uhuru yatumike kuimarisha
ugatuaji wa madaraka kwa
wananchi kwa maendeleo yao.
Alisema, Serikali iliamua kutenga
siku maalumu kuadhimisha
sherehe hizo kila mwaka ili
kuwahabarisha wananchi juu ya
umuhimu wa serikali za mitaa,
nafasi na wajibu wao kwa
serikali za mitaa, pia kuwahimiza
wananchi kuhusu utekelezaji wa
shughuli za maendeleo kwa
lengo la kuchochea ukuaji wa
uchumi na kupunguza umasikini.
Alisema Siku ya Serikali za Mitaa
inatoa fursa kwa kila
halmashauri kuonesha shughuli
mbalimbali zinazotekelezwa
katika mamlaka zao.

MKULIMA ATUHUMIWA KUMBAKA MWANAFUNZI

POLISI mkoani Singida
wamemkamata mkulima, Iddi
Ramadhan (20) mkazi wa kijiji
cha Matyuku Singida Vijijini, kwa
tuhuma za kumbaka mwanafunzi
wa shule ya sekondari na
kumsababishia maumivu makali.
Kamanda wa Polisi mkoani
humo, Celina Kaluba, amesema,
Ramadhan alikamatwa Juni 18
mwaka huu saa moja jioni katika
kitongoji cha Makyunje, Kata ya
Mtamaa tarafa ya Unyakumi
Manispaa ya Singida.
Amesema, mtuhumiwa anadaiwa
kumkamata kwa nguvu binti
huyo mwenye miaka 15, kumziba
mdomo na kumkokota hadi
kichakani na akamvua nguo yake
ya ndani na kumfanyia unyama
huo.
Kamanda Kaluba amesema, mara
baada ya kukamilika kwa
upelelezi, mtuhumiwa
atafikishwa mahakamani kujibu
tuhuma inayomkabili.
Katika tukio lingine, Kaluba
amesema, Polisi wamemkamata
mkulima mkazi wa Mang'onyi,
Singida Vijijini, Saidi Msengi (22)
kwa tuhuma ya kumgonga kwa
pikipiki mwendesha baiskeli,
Polino Michael na kusababisha
kifo chake.
Alieleza kuwa siku ya tukio,
mtuhumiwa alikuwa akiendesha
pikipiki aina ya Sanlag T.708 BRP
na alimgonga mwendesha
baiskeli huyo Michael (50)
mkulima na mkazi wa kijiji cha
Matare.
Alisema, Polino alifariki dunia
akiwa njiani kwenda hospitali ya
mkoa kupatiwa matibabu.

KUNA UBAYA KATIKA FACEBOOK??

La hasha! Ni matunda ya kukua
kwa utandawazi. Mtanzania asiye
na pasport, leo anaweza akawa
na rafiki Australia ambaye
anakuwa anamjua kila
kinachoendelea katika Jiji la
Sydney. Hakuna gharama kubwa,
anajua yote kwa mtindo wa
kuchati kwenye ukurasa wa
Facebook.
Mtanzania akiwa nje ya nje,
akitaka kujua muhtasari wa kile
kinachoendela nchini kwake,
anaweza kutumia gharama
nafuu, kuulizia mazingira na
usalama wa taifa kupitia ukurasa
wa Facebook. Inapeleka watu
katika ulimwengu mpya,
inazidisha uhalali wa usemi
kwamba dunia ya sasa ni kama
kijiji kimoja.
Inasaidia kuongeza wigo wa
marafiki. Watu wanaweza
kubadilishana mawazo ya kijamii,
pia wakapeana uzoefu kwa
namna mbalimbali.
Inawakutanisha watu kwa njia
ya kipekee na kuwafanya
wazoeane kabla ya kugeuka
marafiki wakubwa.
INA ATHARI GANI KIMAPENZI?
Facebook imekuwa ikiwafanya
baadhi ya wanaume kuona njia
ya mkato kupata wapenzi wa
mbali. Akaunti yake inajaza
marafiki wa kike, hana mpango
na wanaume wenzake.
Wanakuza wigo wa kunufaika
katika ngono.
Msomaji na rafiki yangu, Shadya
Ismail aliniandikia ujumbe kwa
SMS ambao unasomeka hivi:
“Simu ni tatizo lakini huku
kwenye Facebook nako ni balaa.
Kusema ukweli, mimi nikigundua
mpenzi wangu anatumia muda
mwingi internet lazima
nimfuatilia nijue kinamsumbua
nini.”
Nilipomuuliza kwanini, alijibu:
“Hakuna amani Facebook.
Mwanaume anaomba urafiki kwa
mwanamke na anamkubalia.
Wakikutana online wanachati,
wanakubaliana baadhi ya vitu na
ikiwezekana wanapanga mpaka
miadi ya kukutana. Amini
kwamba hayo yapo na kuna
watu ni mfano.”
Nikamuomba ufafanuzi:
“Mapenzi ya siku hizi
hayatabiriki, nadhani ndiyo
maana tunaambiwa hizi ni
nyakati za mwisho. Watu
hawajuani lakini wanazoeana
kwa kuchati kisha wanakuwa
wapenzi. Nasema kwa kujiamini
kwa sababu nimetongozwa na
wengi.”
Anasimulia alivyotongozwa:
“Kuna wanaume watatu
waliniomba urafiki kwenye
Facebook. Mimi nikikuta ombi
nakubali. Siku tukikutana online,
tunachati vizuri lakini maswali
mengi yanakuwa yale binafsi
zaidi, yaani kama vile mtu
anataka kukujua sana.
“Nashindwa kutilia hofu,
kwahiyo najibu. Mwisho wa yote
anamalizia kwa kukutaka
kimapenzi. Watu watatu
wamenitongoza na kusitisha
urafiki nao. Ninao marafiki
wawili wa kike, mmoja amewahi
kulala kimapenzi na jamaa
aliyekutana naye Facebook,
alipopata penzi alianza mbele.
“Mwingine mpaka leo
anaendelea na mpenzi wake
ambaye walikutana Facebook.
Lakini huyo mpenzi wake ni
mume wa mtu, kwahiyo
wanaibana. Hapo utaona ni kwa
namna gani fursa za watu
kukaribiana kimapenzi
zimeongezeka hasa baada ya
Facebook kuchanua.”
SHADYA ANASEMA KWELI
Ni ukweli kwamba Facebook
inaumiza watu kwenye mapenzi.
Idadi ya watu wanaoanzisha
uhusiano mpya ni kubwa kila
siku kupitia kurasa hizo.
Uaminifu umekuwa ukipungua
na wasiwasi wa watu kwa
wapenzi wao ni kubwa.
Ninao mfano wa jamaa mmoja
ambaye kila anapofungua
ukurasa wa mwenzi wake, yeye
hukimbilia kuangalia marafiki
wapya ambao amewasajili.
Huumizwa mno anapogundua
kuna midume imo kwenye
orodha. Wanagombezana lakini
ushahidi wa kusaliti haupo.
Mwingine yeye hufuatilia namna
mwenzi wake anavyojadiliana na
marafiki zake katika mada
mbalimbali. Akiona picha ya
mpenzi wake imesifiwa mno na
mwanaume, anahoji:“Huyu
mbona amekusifia sana, ni nani
wako? Lazima mtakuwa
mnajuana, haiwezekani iwe hivi
hivi.”
SULUHISHO
Kila mmoja anatakiwa aishi kwa
maumivu ya mwenzi wake. Ni
vizuri pia akawa na uelewa
mpana kwamba hakuna kitu
kibaya kama kumfanya
mwenzako kuwa na wasiwasi na
wewe. Fanya kila uwezalo lakini
hakikisha mpenzi wako
anakuamini muda wote.
Atakuamini kama humpi sababu
ya kukutuhumu. Haoni tatizo
Facebook, rafiki mwenye
maneno yasiyofaa, jaribu
kumpotezea mapema.
Anapofungua ukurasa wako,
hakuti kitu kibaya zaidi ya
marafiki ambao mazungumzo ni
ya kawaida.
Kwanini ulegee kwa kuchati peke
yake? Onesha msimamo. Kama
wewe ni bachela si vibaya
ukianzisha uhusiano lakini ikiwa
una mwenzi wako, epuka.
Kumbuka kwamba jinsi ilivyo
kwako kupata mpenzi, naye
hivyo hivyo ni rahisi kunasa
wake. Unaona hatari iliyopo?
Uaminifu siyo tu kwamba ni kitu
muhimu, bali pia ni nguzo ya
uhusiano wowote ule. Ukiwa
chanzo wewe ukateleza,
utaachwa au ukisalitiwa
itakuuma na hata uamuzi
utakaouchukua, hautaweza
kufidia maumivu uliyoyapata.

BEI YA MAFUTA YA TAA KUPANDA MARA 7

MAFUTA ya taa na maji ya
kunywa ya chupa yatapanda bei
kutokana na uamuzi wa Serikali
kupandisha ushuru wa bidhaa
hizo.
Kupanda kwa mafuta ya taa ni
dhahiri kutawasononesha
Watanzania wengi hasa vijijini,
lakini Serikali imejitetea kuwa
uamuzi huo umechukuliwa ili
kuepukana na uchakachuaji
mafuta, ambao umeelezwa kuwa
unaididimiza nchi kiuchumi.
Akiwasilisha Muswada wa Sheria
ya Fedha mwaka 2011, Naibu
Waziri wa Fedha, Pereira Silima,
alisema jana kuwa Serikali
imeongeza ushuru wa bidhaa
kwa mafuta ya taa kutoka Sh 52
hadi Sh 400.30.
Uamuzi huo unaondoa tofauti
iliyokuwapo kati ya bei ya dizeli
na bei ya mafuta ya taa na pia
utadhibiti uchakachuaji wa dizeli
ambao hufanywa na
wafanyabiashara kwa
kuchanganya dizeli na mafuta ya
taa, ili kujipatia faida kubwa, kwa
kuwa kodi au bei kwenye mafuta
ya taa ni ndogo.
Eneo hilo la kupandisha bei ya
mafuta ya taa lilipokewa kwa
hisia tofauti na wabunge
ambapo Mbunge wa Bariadi
Magharibi, Andrew Chenge (CCM)
alipongeza hatua hiyo kwa
maelezo kuwa bei ndogo ya
mafuta hayo ilikuwa inanufaisha
watu wachache hasa
wafanyabiashara.
Lakini Mbunge wa Mbozi
Mashariki, Godfrey Zambi (CCM),
alitaka Serikali isipandishe
ushuru wa mafuta ya taa, kwani
ndiyo yanategemewa na
wananchi wengi vijijini.
Amesema, kisingizio cha
kupandisha ushuru huo kwa
kuogopa wachakachuaji,
kinaonesha dhahiri kuwa Serikali
imeshindwa kuwadhibiti
wachakachuaji hao.
Kwa upande wa maji ya kunywa
ya chupa, kinywaji hicho
kimewekwa kwenye kundi la
vinywaji baridi ambavyo ushuru
wake utapanda kutoka Sh. 63,
hadi Sh. 69 kwa lita. Uamuzi huo
utapandisha bei ya maji ya
kunywa ya chupa kama ilivyo
kwa soda na juisi.
Eneo hilo lilipata upinzani kutoka
kwa wabunge, akiwamo
Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha
na Uchumi, Dk. Abdallah Kigoda,
ambaye wakati akiwasilisha
maoni ya Kamati hiyo, alisema
maji ya kunywa ya chupa
yasiongezwe ushuru.
“Tunaishauri Serikali kutoongeza
ushuru kwa bidhaa hizo, kwani
yanatumika na wananchi wengi
wa vijijini na mijini … ni bidhaa
muhimu na ya lazima,” alisema
Kigoda.
Dk. Kigoda amesema, bidhaa hiyo
ya maji imesaidia kupunguza
maambukizi yaliyokuwa
yakisababishwa na maji yasiyo
salama katika baadhi ya maeneo
nchini.
Chenge katika eneo hilo, alisema
maji ya chupa kutokana na
kuuzwa bei ya chini wananchi
wengi wa vijijini wanayatumia
na kupunguza magonjwa ya
kuhara, hivyo yasiongezwe
ushuru.
Katika Muswada huo wa fedha,
Serikali pia imepunguza kwa
kiwango cha asilimia 50 tozo za
mamlaka mbalimbali, ikiwamo
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma
za Maji na Nishati (EWURA),
Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri
wa Nchi kavu na Majini (Sumatra)
na Shirika la Viwango (TBS)
kwenye bidhaa za mafuta.
Amesema, kwa upande wa tozo
za aina hiyo zinazotozwa na
taasisi zingine kama Shirika la
Kusafisha Mafuta (Tiper),
Mamlaka ya Mapato (TRA) na
Mamlaka ya Bandari (TPA), Silima
alisema mikataba na hati husika
zitafanyiwa marekebisho ili
kutekeleza hatua hiyo ya Serikali
ya kupunguzo tozo hiyo kwa
asilimia 50.
Pia alisema ushuru wa mafuta ya
petroli kwa sasa na tozo zote
zitalipwa kwa kutumia sarafu ya
Tanzania au fedha za kigeni
zinazoweza kubadilishwa katika
shilingi ya kitanzania, ambayo
kwa mujibu wa utaratibu wa
Benki Kuu ya Tanzania (BoT),
malipo hayo yanaruhusiwa kwa
dola ya Marekani pekee.
Kuhusu kiwango cha faini ya
makosa ya usalama barabarani,
Serikali imepunguza kiwango
hicho kutoka Sh. 50,000 ya awali
hadi Sh. 30,000.
Amesema lengo la hatua hiyo ni
kuongeza adhabu kwa
watakaovunja sheria za
barabarani, ili kupunguza
ongezeko la ajali.
Hata hivyo, kiwango hicho
kiliendelea kupingwa na
wabunge na kambi ya Upinzani
ikitaka kiwango cha awali cha Sh.
20,000 kiendelee kwani Sh.
30,000 ni kubwa. Nayo Kamati ya
Fedha na Uchumi ilipinga kiasi
hicho na kutaka kishuke hadi Sh.
25,000.

NAPE AMPONGEZA MBOWE KURUDISHA SHANGINGI

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa
Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya
CCM, Nape Nnauye,
amempongeza Kiongozi wa
Kambi ya Upinzani bungeni,
Freeman Mbowe, kwa kusikia
mwito wa chama hicho na
kuamua kurudisha gari la Serikali
alilokuwa akilitumia.
Nape ambaye yupo katika ziara
ya kutembelea vyombo vya
habari nchini, amemtaka Mbowe
kuendelea kutekeleza mwito wa
CCM wa kuhakikisha wafanyakazi
wa Chadema, akiwamo Katibu
Mkuu wa chama hicho, Dk.
Willibrod Slaa, wanalipa kodi
inayotokana na kipato chao
(PAYE).
Nape alitoa kauli hiyo jana
alipokuwa akijibu swali baada ya
kuzungumza na uongozi wa
Kampuni ya Tanzania Standard
Newspapers Ltd (TSN),
inayochapisha magazeti ya Daily
News, Sunday News, HABARI LEO
na HABARILEO Jumapili.
“Anaona aibu kutembelea gari
lililonunuliwa na walipa kodi
wakati Chadema hailipi kodi,
ndiyo maana karudisha kwa
kukosa uhalali wa kulitumia, ni
vema atekeleze mwito wa kulipa
kodi na akimaliza, tutamwambia
mengine ili wajisafishe,” alisema
Nape.
Alikumbusha kuwa CCM ndiyo
iliyoanzisha hoja ya Mbowe
kurudisha gari la Serikali
analotumia. "Mtakumbuka
Chadema walikwenda
Sumbawanga na kuwaambia
wananchi kuwa Waziri Mkuu,
Mizengo Pinda, anatembelea gari
la kifahari.
“Lakini nilipokwenda kule
(Sumbawanga), nilifafanua kwa
wananchi kuwa Mbowe baada ya
kupata cheo cha Kiongozi wa
Upinzani Bungeni, alichukua gari
la gharama kubwa mara tatu ya
gari la Waziri Mkuu,” alisema
Nape.
Kutokana na gharama za gari
hilo la Mbowe, Nape alikumbusha
kwamba alimtaka Mbowe
alirudishe serikalini, ili apewe
gari la gharama ndogo na
kumshukuru kwa kutekeleza
mwito huo juzi alipotangaza
kulirudisha.
Alifafanua, kwamba amekuwa
akiwataka Chadema kuishi kwa
kauli zao na kuepuka kusema
mambo ambayo wao wenyewe
hawayaamini wala
hawayatekelezi.
“Wanapiga kelele watu walipe
kodi, lakini TRA (Mamlaka ya
Kodi), imesema Chadema
haijawahi kulipa kodi tangu
imeanzishwa,” alisema Nape.
Akieleza zaidi tabia hiyo ya
Chadema, ya kusema
wasichotenda, Nape alisema
Mbowe pia aliagiza magari
yaliyotumika na kuyatumia
wakati wa kampeni na baada ya
uchaguzi.
Kwa mujibu wa Nape, Mbowe
alilazimisha Chadema itumie
ruzuku, ambayo ni fedha ya
Serikali, kununua magari hayo
aliyoyatumia huku akijua wazi
kuwa kuna sheria inayokataza
Serikali kununua vitu
vilivyotumika.
Nape pia aliutaka uongozi wa
TSN kuendelea kuandika ukweli
na kuepuka habari zilizotiwa
chumvi na pia iibue maovu hata
ndani ya Serikali, ili kuisaidia
kutekeleza Ilani ya CCM.
Akijibu hoja ya Kaimu Mhariri
Mtendaji wa TSN, Mkumbwa Ally,
kuhusu kampuni hiyo kuidai
Serikali madeni makubwa, Nape
alisema atalifikisha hilo katika
vikao vya chama ili Serikali
itekeleze wajibu wake kwa
kulipa matangazo iliyoyatoa.

Tuesday, June 14, 2011

MKULO;SINA UWEZO WA KUONDOA POSHO

Wakati wanaharakati wakipinga,
Waziri wa Fedha, Mustafa Mkulo,
amesema hana uwezo wa
kuondoa posho za Mbunge wa
Kigoma Kaskazini (Chadema),
Zitto Kabwe, na wenzake wa
NCCR- Mageuzi wanaotaka
ziondolewe.
Akizungumza mjini
Dodoma jana, Mkulo alisema
Baraza la Mawaziri pekee ndilo
lenye uwezo wa kutengua sheria
hiyo na si yeye hivyo
wanaomtaka azihamishe
hawajui wanachosema.
" Mimi Mkulo sina uwezo wa
kubadilisha maamuzi ya baraza la
mawaziri hata siku moja, suala
likishaamriwa kule mtu binafsi
huna uwezo wa kulitengua,
labda niende kwenye baraza hilo
nijenge hoja wakubali,” alisema.
Katika hatua nyingine, Mkulo
alishangaa hatua ya wabunge
wanaokataa posho hizo
zipelekwe kwenye majimbo yao
badala ya kuiachia serikali
uamuzi.
" Kama wanataka zifutwe
waseme, lakini kusema ziende
sehemu fulani haina maana,
kama kweli wanataka kubana
matumizi waseme posho hizi
zifutwe na wafuate taratibu
maana ziko kwa mujibu wa
sheria za nchi,”alisisitiza Mkulo.
" Zitto ni mjumbe wa kamati ya
uongozi ya Bunge kama kweli
hataki hizi posho angesema kule
zikatwe sasa mbona alishiriki
kuzipitisha? "alihoji.
Wabunge wa Chadema na
wengine wanne wa NCCR-
Mageuzi wote kutoka majimbo
ya Mkoa wa Kigoma, wanataka
posho hizo zifutwe.
Akizungumzia posho hizo za
vikao, Mbunge wa Vunjo (TLP),
Agustine Mrema, alisema kwa
kuwa serikali ilishatangaza katika
bajeti yake kuwa itapunguza
posho zisizo za lazima, basi
itaangalia kama posho za
wabunge nazo hazina ulazima.
" Mimi naunga mkono posho
zisizo za lazima ziondolewe,
kama serikali itaona posho za
wabunge si za lazima na
ikaziondoa mimi sina neno,
wakiona mbunge anaweza kuja
hapa Dodoma na akafanya kazi
zake bila kuhitaji hiyo posho
sawa mimi nasubiri uamuzi wa
serikali,” alisema.
Mbunge wa Wawi (CUF), Hamad
Rashid, alisema kuwa: " Katiba
inatamka wazi kwamba mtu
akifanya shughuli hii malipo yake
ni haya sasa tatizo ni nini."
Alisema kama wanaopokea
posho hizo wanaona hawana
haja nazo waandike hundi na
kuzirejesha zilikotoka badala ya
kupiga kelele kwenye vyombo
vya habari.
" Hizo ni cheap politics (siasa
uchara) ambazo mimi binafsi
sizitaki na kamwe sitazishabikia,
mbona wanapokwenda kwenye
halmashauri kule wanasaini
posho iweje wakija huku ndipo
waseme hawazitaki, maoni
yangu ni kwamba tukiamua
kubadili sheria na kuziondoa
sawa sitakuwa na tatizo, lakini
kwa kuwa sasa hivi ziko kisheria
tatizo linatokea wapi,” alisema
Rashid.
Spika wa Bunge, Anne Makinda,
alisema kuna watu wanapotosha
kuwa mshahara wa mbunge ni
zaidi ya milioni saba wakati
mshahara halisi ni Sh. milioni 2.5
na wanakatwa Sh. 900,000 kila
mwezi kwa ajili ya mikopo ya
magari waliyochukua.
KWA HABARI ZAIDI SOMA GAZETI LA NIPASHE LA LEO TAREH 13 JUNE

Monday, June 13, 2011

CLINTON URGES AFRICA TO ABANDON GADDAFI

U.S. Secretary of State Hillary
Clinton has called for African
nations to sever ties with Libyan
leader Moammar Gadhafi and
demand his removal.
Speaking from a lectern where
Gadhafi has often addressed
African assemblies, the secretary
of state acknowledged the
Libyan leader’s influence in the
53-member body. But she urged
African leaders to stand up for
the organization’s democratic
ideals and take the lead in
demanding his ouster.
"I know it is true over many
years, Gadhafi played a major
role in providing financial
support for many African nations
and institutions, including the
African Union, but it has become
clearer by the day he has lost his
legitimacy to rule, and we are
long past time when he can or
should remain in power," said
Clinton.
In the first-ever address by a U.S.
secretary of state to the African
Union, Clinton called for the
continent’s leaders to isolate
Gadhafi diplomatically.
"I urge all African states to call for
a genuine cease-fire and to call
for Gadhafi to step aside," she
said. "I also urge you to suspend
the operations of Gadhafi’s
embassies in your countries, to
expel pro-Gadhafi diplomats, and
to increase contact and support
for the [rebel] Transitional
National Council."
Speaking to an A.U. plenary hall
packed with diplomats and
dignitaries, Clinton hailed the so-
called "Arab Spring" bringing
about democratic reforms in
parts of North Africa and the
Middle East. She praised people in
countries long ruled by dictators
who are now demanding new
leadership, often, as she put it,
“at the top of their lungs."
"In places where jobs are scarce
and a tiny elite prospers while
most of the population struggles,
people, especially young people,
are channeling their frustration
into social, economic and political
change," said Clinton. "Their
message is clear to us all, the
status quo is broken, the old
ways of governing are no longer
acceptable, it is time for leaders
to lead with accountability, treat
their people with dignity, respect
their rights, and deliver economic
opportunity. And if they will not,
then it is time for them to go."
In what was billed as a major
policy address, Clinton received
applause for acknowledging the
plight of African women, calling
them“the hardest-working
women in the world."
"So often what they do is not
included in the formal economy,
it is not measured in the GDP,
and yet if all the women in Africa,
from Cairo to Cape Town decided
they would stop working for a
week, the economies of Africa
would collapse," she said.
Secretary Clinton was due to visit
a number of projects designed to
empower women during the
final day of her Africa tour. But
her visit was abruptly cut short
due to concern about an ash
cloud caused by a volcanic
eruption in neighboring Eritrea.
She flew back to Washington late
Monday.

KATIBA YA ZANZIBAR KUWASILISHWA LEO

WAZIRI wa Fedha wa Serikali ya
Mapinduzi Zanzibar, Omar Yussuf
Mzee leo Jumatano
atawasilisha bajeti ya serikali
kwa mwaka 2011/12 huku
wafanyakazi wa serikali wakiwa
na matarajio ya kuongezewa
mishahara yao.
Katibu wa Baraza la Wawakilishi
Ibrahim Mzee alisema juzi kuwa
bajeti hiyo itasomwa kuanzia saa
10 jioni katika kikao hicho cha
bunge ambacho kitaketi kwa
wiki sita.
“Hatujajua kilichomo kwenye
hotuba ya bajeti, lakini katika
mkutano huo wa Bunge maswali
237 yataulizwa na wawakilishi
na kujibiwa na mawaziri,”
alisema katibu huyo.
Hiyo itakuwa ni bajeti ya kwanza
tangu kuundwa kwa Serikali ya
Umoja wa Kitaifa (GNU)
inayohusisha mawaziri kutoka
vyama vya CCM na CUF. Waziri
Mzee juzi jioni alitarajiwa pia
kuzungumza na waandishi wa
habari juu ya mweleko wa bajeti
hiyo.
Baadhi ya wachambuzi wa
mambo wametaka bajeti hiyo
ijielekeze zaidi kumpunguzia
mwananchi wa kawaida makali
ya maisha, ikiwa ni pamoja na
kupunguza mfumuko wa bei na
pia ijielekeze katika kuboresha
masuala ya kilimo, afya na elimu.
Ili kukifanya kikao hicho
kisikwame kutokana na matatizo
ya umeme, katibu huyo alisema
tayari ofisi yake imeshanunua
jenereta la dharura lenye uwezo
wa kutoa kilovoti 7.25 za umeme
ambalo limenunuliwa kwa
thamani ya Sh milioni 355.
Alisema jenereta hilo litawasili
kisiwani hapa wakati wowote,
“Na pia tumetumia Sh milioni sita
kwa ajili ya kupunguza
mwangwi kwenye ukumbi wa
baraza.”
Tangu kufunguliwa kwa ukumbi
mpya wa baraza la wawakilishi,
wajumbe wa baraza la
wawakilishi wamekuwa
wanalalamika kwa spika kuwa
mawasiliano ndani ya ukumbi
huo ni magumu kutokana na
kuwepo kwa mwangwi pamoja
na kutokuwepo na jenereta la
dharura.

Askofu mkuu Anglikana atakiwa kizimbani

SAKATA la mgogoro wa Kanisa la
Anglikana mkoani hapa
limechukua sura mpya baada ya
Mahakama Kuu Kanda ya Arusha
kutoa hati ya kukamatwa kwa
Askofu Mkuu wa Kanisa hilo
nchini.
Mbali ya hilo pia Mahakama hiyo
awali ilisimamisha shughuli zote
za usimikaji wa Askofu na juzi
pia kutoa hati ya kukamatwa
kwa Askofu aliyesimikwa juzi,
Stanley Hotay.
Kutokana na amri hiyo, iwapo
Askofu Hotay atakamatwa na
kutiwa hatiani kwa kosa la
kukaidi amri ya Mahakama,
huenda akawa amepoteza sifa za
kuwania tena kiti hicho cha
uaskofu kwa mujibu wa taratibu
za kanisa hilo.
Kutolewa kwa hati hiyo na Jaji
Kakusulo Sambo kumekuja siku
moja baada ya juzi Askofu Hotay
kusimikwa kuwa Askofu wa
Kanisa la Anglikana Tanzania
badala ya Dayosisi ya Mount
Kilimanjaro.
Juni 10, Mahakama Kuu hiyo
ilitoa amri ya kuzuia kuapishwa
kwa Askofu Hotay, hadi shauri la
kupinga kusimikwa kwake
lililofunguliwa na waumini
watatu wa Kanisa la St. James
jijini hapa litakaposikilizwa na
kutolewa uamuzi.
Waumini waliofungua kesi hiyo
ni pamoja na Godfrey Mhone
ambaye ni mume wa
mwanamuziki wa injili nchini,
Beatrice Mhone, Lothi Oilevo na
Frank Jacob, ambapo kwa
pamoja wanadai kwamba
uchaguzi uliomweka madarakani
Askofu huyo una mpango
mahsusi wa kukiuka Katiba ya
Kanisa hilo.
Akitoa uamuzi wa Mahakama
hiyo mara baada ya kusikiliza
hoja za pande mbili katika shauri
hilo, Jaji Sambo alisema
ameridhika pasipo shaka
kwamba amri ya Mahakama
aliyoitoa Ijumaa ilipuuzwa.
Alisema katika kosa kama hilo,
sheria iko wazi kushughulikia
watu wanaokiuka amri za
Mahakama.
Alisema kwa vile shauri hilo
lilikuwa halimhusu Dk. Mokiwa,
lakini katika hatua nyingine
tayari amefanya jambo ambalo
limesababisha amri ya Mahakama
isiheshimiwe, “sasa natoa amri
ya Mahakama ya kumtaka Askofu
Mokiwa na Askofu Hotay
wakamatwe haraka sana. Na
uamuzi mdogo wa shauri hili
nitautoa baadaye.
“Kwa sababu huyu tayari
amekwishakuwa Askofu na mtu
akishasimikwa kuwa Askofu ni
kazi kweli kweli kumwondoa,”
alisema Jaji Sambu.
Huku akionekana kuwa mkali, Jaji
Sambu alisema pamoja na
Mahakama hiyo kutoa amri hiyo,
lakini kwa sasa itabidi kuangalia
upya tena namna ya kuendesha
shauri hilo kutokana na
kuapishwa kwa Askofu huyo.
Alisema kabla ya Mahakama
kusikiliza upande wa pili
uliokuwa unalalamikiwa, tayari
ulishamsimika Askofu Hotay
ambapo kwa hatua hiyo, ni sawa
na kupindisha utaratibu wa kesi.
Uamuzi wa kukamatwa kwa
maaskofu hao, ulitolewa baada
ya wakili wa upande wa
mashitaka, Meinrad D’souza,
kuwasilisha maombi maalumu
mahakamani hapo ili itoe adhabu
kwa Dk Mokiwa na Hotay,
kutokana na kukiukwa amri ya
Mahakama.
Akisoma uamuzi kwa Kiswahili
kwa takriban saa moja huku
akisikilizwa kwa utulivu na
mamia ya waumini wa Kanisa la
Anglikana waliofurika
mahakamani, hapo, Jaji Sambo
alisema haihitaji elimu ya chuo
kikuu kuona kuwa
walichokifanya maaskofu hao wa
Anglikana kuwa ni kudharau
amri halali ya Mahakama.
Awali wakili D’Souza alisema
kitendo cha Askofu Mokiwa
kumsimika Hotay kimeingilia
uhuru wa Mahakama na
kushusha heshma ya Mahakama
Kuu, kwani ilikishatoa agizo la
kusitishwa kwa shughuli zozote
za kuapishwa Hotay.
D’Souza alisema alichokifanya
Askofu Mokiwa juzi ni kuvuruga
mwenendo mzima wa kesi hiyo,
ambayo inapinga mshitakiwa wa
pili, Hotay kuapishwa kwani umri
wake umegushiwa, na Katiba ya
Anglikana inaeleza wazi kuwa
Askofu anapaswa kuwa na umri
unaoanzia miaka 40 lakini Hotay
ana miaka 38 na hivyo tararibu
zote za uchaguzi zilikiukwa.
Hata hivyo, mawakili wa upande
wa Utetezi, Joseph Thadayo na
Issa Mavura, waliiomba
Mahakama itupilie mbali maombi
ya kuchukuliwa hatua maskofu
Mokiwa na Hotay kwa maelezo
kuwa hawakuingilia mwenendo
wa kesi hiyo.
Thadayo alimkabidhi Jaji Sambo
tamko la Askofu Mokiwa ambalo
linaeleza kilichotokea, kuwa
Hotay alisimikwa kama Askofu
wa Kanisa Anglikana Tanzania si
wa Dayosisi ya Mount
Kilimanjaro.
Mara baada ya uamuzi huo,
Wakili Thadayo alisema ni wa
Mahakama na hivyo hawana
jambo la kufanya zaidi ya
kutekeleza maagizo hayo.

you and i: WE ARE BACK

you and i: WE ARE BACK

WE ARE BACK

tunashukuru kwa kuwa sasa tutaendelea kupeana habari mbalimbali kutoka kila pande ya dunia bila upendeleo ama uoga wowote!